1 |
Basi, ndugu, kwa habari ya nyakati na majira hatuna haja ya kuwaandikia, |
2 |
kwa kuwa mnajua vyema kwamba siku ya Bwana itakuja kama mwivi ajapo usiku. |
3 |
Wakati watu wanaposema, “Kuna amani na salama,” maangamizi huwajia ghafula kama vile utungu umjiavyo mwanamke mwenye mimba wala hawatatoroka. |
4 |
Bali ninyi, ndugu, hamko gizani hata kwamba siku ile iwakute ghafula kama mwivi. |
5 |
Ninyi nyote ni wana wa nuru na wana wa mchana. Sisi si wana wa giza wala wa usiku. |
6 |
Kwa hiyo basi, tusilale kama watu wengine walalavyo, bali tukeshe na kuwa na kiasi. |
7 |
Kwa kuwa wote walalao hulala usiku na wale walewao hulewa usiku. |
8 |
Lakini kwa kuwa sisi ni wana wa mchana, basi tuwe na kiasi, tukijivika imani na upendo kama dirii kifuani na tumaini letu la wokovu kama chapeo. |
9 |
Kwa maana Mungu hakutuita ili tupate ghadhabu bali tupate wokovu kwa njia ya Bwana wetu Yesu Kristo. |
10 |
Yeye alikufa kwa ajili yetu ili kwamba kama tuko macho au tukiwa tumelala tupate kuishi pamoja naye. |
11 |
Kwa hiyo farijianeni na kujengana, kama vile mnavyofanya sasa. |
12 |
Sasa tunawaomba, ndugu, waheshimuni wale wanaofanya kazi kwa bidii miongoni mwenu, wale ambao wana mamlaka juu yenu katika Bwana na ambao wanawaonya. |
13 |
Mkawajali sana katika upendo kwa ajili ya kazi yao. Iweni na amani ninyi kwa ninyi. |
14 |
Nasi twawasihi, ndugu, waonyeni wale wavivu, watieni moyo waoga, wasaidieni wanyonge na iweni na uvumilivu na kila mtu. |
15 |
Angalieni kuwa mtu asilipe ovu kwa ovu, bali siku zote tafuteni kutendeana mema ninyi kwa ninyi na kwa watu wote. |
16 |
Furahini siku zote; |
17 |
ombeni pasipo kukoma; |
18 |
shukuruni kwa kila jambo, kwa maana haya ndiyo mapenzi ya Mungu kwa ajili yenu katika Kristo Yesu. |
19 |
Msiuzime moto wa Roho Mtakatifu; |
20 |
msiyadharau maneno ya unabii. |
21 |
Jaribuni kila kitu. Yashikeni yaliyo mema. |
22 |
Jiepusheni na uovu wa kila namna. |
23 |
Mungu mwenyewe, Mungu wa amani, awatakase ninyi kabisa. Nanyi mhifadhiwe roho zenu, nafsi zenu na miili yenu, bila kuwa na lawama katika Bwana wetu Yesu Kristo. |
24 |
Yeye aliyewaita ni mwaminifu naye atafanya hayo. |
25 |
Ndugu, tuombeeni. |
26 |
Wasalimuni ndugu wote kwa busu takatifu. |
27 |
Nawaagizeni mbele za Bwana mhakikishe kuwa ndugu wote wanasomewa barua hii. |
28 |
Neema ya Bwana wetu Yesu Kristo iwe nanyi. Amen.
|
Swahili Bible 2015 Contemporary |
Copyright ©1984, 1989, 2009, 2015 by Biblica, Inc.® Used by permission |
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
1 Wathesalonike 5:1 |
1 Wathesalonike 5:2 |
1 Wathesalonike 5:3 |
1 Wathesalonike 5:4 |
1 Wathesalonike 5:5 |
1 Wathesalonike 5:6 |
1 Wathesalonike 5:7 |
1 Wathesalonike 5:8 |
1 Wathesalonike 5:9 |
1 Wathesalonike 5:10 |
1 Wathesalonike 5:11 |
1 Wathesalonike 5:12 |
1 Wathesalonike 5:13 |
1 Wathesalonike 5:14 |
1 Wathesalonike 5:15 |
1 Wathesalonike 5:16 |
1 Wathesalonike 5:17 |
1 Wathesalonike 5:18 |
1 Wathesalonike 5:19 |
1 Wathesalonike 5:20 |
1 Wathesalonike 5:21 |
1 Wathesalonike 5:22 |
1 Wathesalonike 5:23 |
1 Wathesalonike 5:24 |
1 Wathesalonike 5:25 |
1 Wathesalonike 5:26 |
1 Wathesalonike 5:27 |
1 Wathesalonike 5:28 |
|
|
|
|
|
|
1 Wathesalonike 1 / 1Wa 1 |
1 Wathesalonike 2 / 1Wa 2 |
1 Wathesalonike 3 / 1Wa 3 |
1 Wathesalonike 4 / 1Wa 4 |
1 Wathesalonike 5 / 1Wa 5 |